Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge amewaapisha wakuu wa wilaya za Dodoma mjini na Bahi mkoani Dodoma huku akiwataka wakuu hao kuacha kukaa ofisini badala yake wafike vijijini ili kubaini changamoto za wananchi ikiwa ni pamoja na kutatua migogoro ya ardhi ambayo imekuwa kero kwa wananchi.
Kwa upande wake mkuu mpya wa Dodoma Patrobas Katambi ameweka wazi vipaumbele vyake ikiwa ni pamoja na kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa.
Ещё видео!